Loading...

SORRY MADAM -Sehemu ya 3 & 4 (Destination of my enemies)

 
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Yule mshenzi amepewa uwaziri wa ulinzi Tanzania?”
“Mungu wangu………ana sifa gani za yeye kuwa waziri?”
“Ndio hivyo. Yaani laiti ningejua huyu mchenzi ningemuua tangu tukiwa ndani ya ndege ninaamini kwamba tusinge kuwa tunazungumza mazungumuzo ya kumuuhusu huyu kibwengo mtu”
“Kwa nini usimuue?”
“Mazingira hayakuruhusu, alipelekea kunipa shida ya kutafutwa hapo bendeni kwa hayati Mzee Madiba”
“Ulitokaje tokaje ndani ya ndege?”
Swali la Madam Mery likamfanya Mzee Godwin kurudisha kumbukumbu zake nyuma kwa haraka hadi siku aliyo toka kupambana na Eddy ndani ya ndege na taratibu akaanza kusimulia.

ENDELEA
“Nilipo onekanana sura yangu, iliniazimu mimi kuondoka na kuachana na Edddy kwani endepo ningeendelea kupambana naye ningeingia mikononi mwa askari na ingekuwa ni swala jengine.”
“Nilijichanganya katikati ya askari ambao walikuwa wakikagua watu basi, nikafanikiwa kutoka pasipo wao kugundua kwamba mimi ndio niliye kuwa nimesababisha maafa hayo”

“Sasa uliingiaje ndani ya ndege?”
“Ahaa, nilimtumia njia ya kujificha kwenye mizigo, baada ya kumuona Eddy akiwa anahangaikia usafiri wa kuja nchini Tanzania”
“Aiseee una hatari kweli kweli wewe”
“Weee acha tu, sasa lengo na thumuni la kukuita hapa ninahitaji kuweza kumpoteza Eddy mara moja kwenye huu uso wa dunia. Ila tahadhari ni moja, dogo amekuwa waziri, tena waziri wa ulinzi”

“Kama nilishindwa kumuua kipindi akiwa mtu wa kawaida, basi ujue kazi ya kumuangamiza yeye ni kubwa sana”
Madam Mery akashusha pumzi nyingi huku akimtazama Mzee Godwin anaye onekana kuwa na mawazo mengi kichwani mwake. Mzee Gowin kabla hajaendelea kuzungumza ujumbe mfupi ukaingia kwenye simu yake, taratibu akaanza kuusoma, na tabasamu pana likajijenga usoni mwake ikiwa ni ishara ya furaha
                                                                                         ***
    Kukamatwa kwa mchungaji Mandingo na Madam Glory watu maarufu katika nchi ya Tanzania kukaana kuwashangaza wananchi wengi, vyombo vingi vya habari vilidai kwamba watu hao wamekamatwa na waziri mpya wa ulinzi. Waandishi wengi walifunga foleni kwenye jengo la waziri wa ulinzi wakihitaji kufanya mkotano na waziri huyo ambaye hadi sasa hivi hawamuelewi nini ni maana ya kuwakamata watumishi hao wenye kumsaidia kila mwenye shida mbele ya macho yao
“Muhesimiwa, muheshimiwaa”
Waandishi baadhi walimuuita Eddy alipo kuwa akishuka kwenye gari lake.

“Ni kwa nini umeamua kuwakamata watumishi wa bwana Mchungaji Mandingo na Madam Grory?”
Muandishi mmoja wa gazeti la Habari Sasa alimuuliza waziri Eddy Godwin
“Siwezi kuzungumza lolote kwa sasa, ila huo ni mwanzo tu waujibikaji wangu, ila kazi inaendelea”
Eddy alijibu na kuomba kupishwa kukiwahi kikao cha wakuu wa jeshi la polisi ambao tayari wamesha wasili kwenye ukumbi wa mikutano tangu saa mbili asubuhi. Eddy hakuwa na haja ya kwenda ofisisni kwake moja kwa moja akaelekea katika ukumbi wa mkutano, Akawakuta wakuu wote wa jeshi la polisi, kutoka mikoani mwote wakiwa wanamngojea.
“Wakubwa zangu shikamoni”

Waziri Eddy alisalimia kwani watu wote waliomo ndani ya ofisi yake wamempita umri mkubwa sana na wengine ni sawa na baba zake. Kila mmoja akaitikia salamu hiyo
“Samahani kwa kuchelewa kuweza kuwahi kwenye kikao, ila hakuna kilicho haribika.”
“Lengo la kuwaita hapa ninahitaji kujadiliana nanyi, kuhusiana na watendaji wenu katika mikoa yenu.”
“Napenda kujua ni nini kilicho pungua kwenye idara yenu kuanzia madai munayo idaia serikali ili yaweze kulipwa haraka iwezekanavyo”
Eddy alizungumza na kuwatazama wakuu wote walio fika kwenye kikao hichi. Mmoja akanyoosha kidole na kuzungumza.

“Mkuu hapo kinacho tusumbua kwanza ni ufinyu wa mishahara kwa vijana wetu, mishahara kupungua na mazingira mabaya ya nyumba wanazo ishi kambini. Magari ni machakavu, piklikipi za doria ni chache kwahiyo inapelekea vitendo vingi vya uhalifu kufanyika katika nchi yetu”
“Asante nitalishuhulikia, mwengine”
“Muheshimiwa sisi tunahitaji sihasa isiingizwe kwenye majeshi kama hawa wezako walio pita kwa maana walikuwa wakituletea siaaa kwenye kazi zetu na kujikuta vijana wetu wakishindwa kufanya kazi kwa amani, jambo linalo pelekea uhalifu kuzidi kuongezeka”

“Asante baba yangu, ngoja niwatoe hofu kwenye hili. Mimi si mwana siasa na wala sina chama ila ninanchi. Labda nitoe rai moja kwenu. Musidanganyike na mwanasiasa yoyote. Yoyote ambaye ataingia kwenye jeshi la polisi, kama muhalifu hakikisheni munamuua na si kumuacha hai”
Wazo la waziri Eddy Godwin likawafanya wakuu wengi wa jeshi kushangaa kwani hawakutegemea kupata wazo kama hilo kwenye kikao hicho.
“Muheshimiwa kumbuka kwamba sisi ni jeshi la polisi kazi yetu ni kulinda wananchi na mali zao. Sasa unapo sema tuwaue inakuwa ni kazi kidogo kwetu huoni kwamba tutakuwa na sifa mbaya?”

“Samahani baba yangu kwa majibu haya nitakayo kupa, ila kiukweli hadi sasa hivi nyinyi muna sifa mbaya mbaya mbaya zaidi ya shetani na ubaya wake. Wahalifu wengi tupo nao huku juu serikalini. Wanawatumikisha vijana wadogo wanakamatwa na kufungwa, ila muzizi ipo inaendelea kuzalisha matatizo mengine mengi kwenye ngi hii. Sasa hii ni amri wala sio ombi, na lolote litakalo fanyika basi mimi nitakuwa muwajibikaji katika kuyajibu hayo ICC”
Baadhi ya wakuu wa polisi wakapiga makofi kwa ujasiri anao uonyesha kijana mdogo mwenye mamlaka makubwa kwenye nchi hii.
“Tumekuelewa muheshimiwa”
“Asanteni kwa kunielelewa, ila wapeni tahathari vijana wenu. Nitakuwa nikizunguka zunguka kwenye kila mkoa na vituo vyote kisiri pasipo wao kujua, endapo nitaumdua kuna ubadhilifu wowote kwa wananchi basi, kijana huyo au hao watawajibika katika hilo. Asanteni kwa muda wenu” 

***
“Mbona unatabasamu?”
Madam Mery alimuuliza mzee Godwin
“Kijana wangu, niliye potezana naye muda yupo hai”
“Ni nani?”
“John”
“John yupi?”
“Yule aliye kua mwanafunzi wako”
Furaha ya mzee Godwin na Madam Mery ikazidi kuongezeka kwani mtu waliye kuwa wanamtegemea kwenye mipango yao wamepata ujumbe wake kwa njia ya simu.
“Sasa yupo wapi?”
“Yeye mwenyewe hakuniambia kwamba yupo wapi ila atanijulisha kwamba yupo wapi”
“Sawa”
“Ila itabidi kuunda kikosi chenye nguvu na safari hii, Eddy nilazima afee”
Mzee Godwin alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake, macho yake akiwa amemtazama Madam Mery.

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright KISWAGA BLOG
Back To Top